- Oct 22,2021
- General
Discover the newest articles and updates from our blog, covering a variety of engaging topics.
Leo Februari 19, 2021 Mahakama ya Rufaa Mkoani Mwanza, imesikilizwa kesi ya rufaa ambayo ilifunguliwa na UTPC na Halihalisi publishers dhidi ya sheria ya huduma za vyombo vya Habari (MSA), 2016 baada ya Mahakama kuu kutoa hukumu yake mwaka 2018.
Katika rufaa hii, UTPC na Halihalisi wamewakilishwa na mawakili Edwin Aron Hans na Jeremiah Mtobesya.
Mawakili wa UTPC na Halihalisi waliwasilisha rufaa hiyo mbele ya majaji wa Mahakama ya rufaa mkoani Mwanza na mbele ya mawakili wa serikali.
Mwaka 2017, UTPC na Halihalisi Publishers walifungua kesi ya kikatiba dhidi ya Mwanashiria Mkuu wa Serikali kupinga sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari ambayo inakiuka misingi ya kikatiba kuhusu Uhuru wa Kujieleza na Uhuru wa Vyombo vya Habari.
Baada ya majadiliano marefu, Majaji wa rufani wameeleza kutoa maamuzi ya rufaa hiyo baada ya siku chache kutoka leo.
Notisi hii imetolewa kwa wanachama wote wa UTPC, kwa mujibu wa kifungu namba 14 (Viii) cha katiba ya UTPC, kwamba Mkutano Mkuu wa wa UTPC kwa mwaka 2020 utafanyika tarehe 16 na 17 Novemba 2020, kwenye Ukumbi wa Flomi Hotel, Morogoro.
Ajenda zitakazojadiliwa kwenye mkutano huo ni;
KufunguaMkutano
KuthibitishaajendazaMkutano
Kupokea,kujadilinakuidhinishamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka 2019
YatokanayonamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka2019
Kupokea,kujadilinakupitishataarifayaUtekelezajinataarifayaukaguzi wa hesabu za UTPC kwa mwaka 2019
UchaguziwaWajumbewaBodiyaWakurugenzi
MengineyokwaidhiniyaMwenyekiti
KufungaMkutano
Imetolewa na
Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC
Abubakar Karsan
UTPC ipo kwenye maandali ya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa UTPC utakaofanyika tarehe 16 na 17 mwezi Novemba mkoani Morogoro.
Pamoja na mambo mengine, moja ya maandalizi yaliyokamilika ni Fomu ya kugombea ujumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC. Fomu hii zinapatikana katika ofisi za Press Clubs zote nchini pamoja na kwenye tovuti ya UTPC.
Kwa kuona umuhimu wa matibu kwa wanachama wa klabu za waandishi wa habari, UTPC ilifanya mazungumzo na mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) kwa lengo la kutengeneza kifurushi au mpango maalumu wa matibabu kwa waandishi wa habari ambao ni wanachama wa klabu za waandishi wa habari.
Katika mazungumzo hayo, UTPC na NHIF walikubaliana kwamba kila mwanachama atachangia Tsh. 100,000/= kwa mwaka akiwa peke yake bila mtegemezi, na kama atahitaji kuweka mtegemezi ambaye umri wake ni zaidi ya miaka 18 atachangiwa Tsh. 100,000/= na mtoto atachangiwa Tsh. 50,400/= kwa mwaka.
Baada ya mazungumzo hayo kukamilika, klabu zote zilijulishwa kuhusu fursa hiyo ya matibabu ambayo ilitengenezwa mahususi kwa ajili ya waandishi wa habari.
Klabu zilianza kuhamasisha wanachama wake na kukusanya michango kwa ajili ya kuwakatia bima ya afya.
Jumla ya klabu 11 zimekamilisha chakato wa kuwakatia bima ya afya wanachama wake kama inavyoonekana katika orodha hapa chini
Central Press Club
Geita Press Club
Kigoma Press Club
Mwanza Press Club
Mbeya Press Club
Rukwa Press Club
Shinyanga Press Club
Simiyu Press Club
Zanzibar Press Club
Katavi Press Club
Dar City Press Club
Kwa sasa hakuna klabu itakayoendelea na mchakato huu mpaka mwakani. Hivyo klabu ambazo hazijakamilisha mchakato huu, zitapewa nafasi ya kukamilisha shughuli hii mwaka 2021.
Mkutano Mkuu wa UTPC uliofanyika tarehe 15 na 16 Septemba 2017 mkoani Tanga, ulifanya mabadiliko ya katiba yake kuhusu muda wa ukomo wa viongozi wa klabu kuwapo madarakani kutoka miaka mitatu hadi miaka mitano kama inavyoonekana katika katiba ya UTPC kipengele namba 15 (C).
Kwa mujibu wa azimio namba 8.3 la Mkutano Mkuu wa dharura uliofanyika Dodoma terehe 23/08/2013, wajumbe waliazimia kwamba klabu zote zifanye uchaguzi wao mapema kabla ya uchaguzi wa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ambapo wajumbe wake huchaguliwa kutoka miongoni mwa viongozi wa juu wa Klabu za Waandishi wa Habari.
Katika kikao cha 33 cha Bodi ya Wakurugenzi kilichofanyika tarehe 20/11/2019 mkoani Dodoma, kilipitisha azimio namba 5.2.4.1 ambalo lilizitaka klabu zote ziwe zimefanya uchaguzi wa viongozi wake mpaka kufikia tarehe 30 Juni 2020 ili kupisha uchaguzi wa Mkuu wa Serikali na uchaguzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC.
Hata hivyo kutoka na mlipuko wa ugonjwa wa COVID19, Bodi ilisogeza mbele muda wa chaguzi za klabu mpaka kufikia tarehe 30 Septemba 2020.
Baada ya maagizo haya kutolewa na Bodi ya Wakurugenzi, klabu zilianza kufanya chaguzi zake katika vipindi tofauti tofauti, na ifuatayo ni orodha ya klabu ambazo zimeshafanya chaguzi zake;
Central Press Club
Kigoma Press Club
Njombe Press Club
Mwanza Press Club
Geita Press Club
Songwe Press Club
Rukwa Press Club
Katavi Press Club
Mara Regional Press Club
Simiyu Press Club
Shinyanga Press Club
Mtwara Press Club
Lindi Press Club
Kagera Press Club
Mbeya Press Club
Arusha Press Club
Manyara Press Club
Klabu zilizobaki bado zinaendelea na mchakato wa kufanya chaguzi zake na pindi wakatakapo maliza taarifa yake itaandaliwa.