Event

Latest from our posts

Discover the newest articles and updates from our blog, covering a variety of engaging topics.

Blog

WAFANYAKAZI WA UTPC WAJENGEWA UWEZO

Mafunzo ya ndani ya siku tatu kwa wafanyakazi wa UTPC ya namna bora ya kufanya Tathmini na Ufuatiliaji wa miradi (Monitoring and Evaluation) yamemalizika katika ofisi za UTPC.
Mafunzo haya yamewezeshwa na shirika la IMS ambalo UTPC inafanya nalo kazi kupitia mradi wa ushirikiano unaolenga kuzingea uwezo taasisi za kihabari nchini kushiriki kwenye ushawishi wa kuboresha uhuru wa habari, uhuru wa wananchi kupata taarifa na upatikanaji wa haki za msingi.
Mashirika mengine yanayotekeleza mradi huu na ambayo yamejengewa uwezo ni MISA TAN, TAMWA, MULIKA na ZANZIBAR YOUTH FORUM
Read More
Blog

MAHAKAMA KUU YA RUFAA MWANZA ITATOA MAAMUZI YA RUFAA YA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI (MSA) 2016 SIKU CHACHE ZIJAZO

Leo Februari 19, 2021  Mahakama ya Rufaa Mkoani Mwanza, imesikilizwa  kesi ya rufaa ambayo ilifunguliwa na UTPC na Halihalisi publishers dhidi ya sheria ya huduma za vyombo vya Habari (MSA), 2016 baada ya Mahakama kuu kutoa hukumu yake mwaka 2018.

 

Katika rufaa hii, UTPC na Halihalisi wamewakilishwa na mawakili Edwin Aron Hans na Jeremiah Mtobesya.

Mawakili wa UTPC na Halihalisi waliwasilisha rufaa hiyo mbele ya majaji wa Mahakama ya rufaa mkoani Mwanza na mbele ya mawakili wa serikali.

 

Mwaka 2017, UTPC na Halihalisi Publishers walifungua kesi ya kikatiba dhidi ya Mwanashiria Mkuu wa Serikali kupinga sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari ambayo inakiuka misingi ya kikatiba kuhusu Uhuru wa Kujieleza na Uhuru wa Vyombo vya Habari.

 

Baada ya majadiliano marefu, Majaji wa rufani wameeleza kutoa maamuzi ya rufaa hiyo baada ya siku chache kutoka leo.

Read More
Blog

NOTISI YA MKUTANO MKUU WA UTPC MWAKA 2020

Notisi hii imetolewa kwa wanachama wote wa UTPC, kwa mujibu wa kifungu namba 14 (Viii) cha katiba ya UTPC, kwamba Mkutano Mkuu wa wa UTPC kwa mwaka 2020 utafanyika tarehe 16 na 17 Novemba 2020, kwenye Ukumbi wa Flomi Hotel, Morogoro.

 

Ajenda zitakazojadiliwa kwenye mkutano huo ni;

  1. KufunguaMkutano

  2. KuthibitishaajendazaMkutano

  3. Kupokea,kujadilinakuidhinishamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka 2019

  4. YatokanayonamuhtasariwaMkutanoMkuuwamwaka2019

  5. Kupokea,kujadilinakupitishataarifayaUtekelezajinataarifayaukaguzi wa hesabu za UTPC kwa mwaka 2019

  6. UchaguziwaWajumbewaBodiyaWakurugenzi

  7. MengineyokwaidhiniyaMwenyekiti

  8. KufungaMkutano

     

     

     

     

Imetolewa na 

Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC

Abubakar Karsan

Read More
Blog

UTPC YATOA FOMU ZA KUGOMBEA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI

UTPC ipo kwenye maandali ya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa UTPC utakaofanyika tarehe 16 na 17 mwezi Novemba mkoani Morogoro.

 

Pamoja na mambo mengine, moja ya maandalizi yaliyokamilika ni Fomu ya kugombea ujumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC. Fomu hii zinapatikana katika ofisi za Press Clubs zote nchini pamoja na kwenye tovuti ya UTPC. 

 

Read More
Blog

KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 11 ZAJIUNGA NA BIMA YA AFYA

Kwa kuona umuhimu wa matibu kwa wanachama wa klabu za waandishi wa habari, UTPC ilifanya mazungumzo na mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) kwa lengo la kutengeneza kifurushi au mpango maalumu wa matibabu kwa waandishi wa habari ambao ni wanachama wa klabu za waandishi wa habari.

 

Katika mazungumzo hayo, UTPC na NHIF walikubaliana kwamba kila mwanachama atachangia Tsh. 100,000/= kwa mwaka akiwa peke yake bila mtegemezi, na kama atahitaji kuweka mtegemezi ambaye umri wake ni zaidi ya miaka 18 atachangiwa Tsh. 100,000/= na mtoto atachangiwa Tsh. 50,400/= kwa mwaka.

 

Baada ya mazungumzo hayo kukamilika, klabu zote zilijulishwa kuhusu fursa hiyo ya matibabu ambayo ilitengenezwa mahususi kwa ajili ya waandishi wa habari.

Klabu zilianza kuhamasisha wanachama wake na kukusanya michango kwa ajili ya kuwakatia bima ya afya.

 

Jumla ya klabu 11 zimekamilisha chakato wa kuwakatia bima ya afya wanachama wake kama inavyoonekana katika orodha hapa chini

 

Central Press Club

Geita Press Club

Kigoma Press Club

Mwanza Press Club

Mbeya Press Club

Rukwa Press Club

Shinyanga Press Club

Simiyu Press Club

Zanzibar Press Club

Katavi Press Club

Dar City Press Club

 

Kwa sasa hakuna klabu itakayoendelea na mchakato huu mpaka mwakani. Hivyo klabu ambazo hazijakamilisha mchakato huu, zitapewa nafasi ya kukamilisha shughuli hii mwaka 2021.

Read More
Blog

KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI 17 ZAKAMILISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAO

Mkutano Mkuu wa UTPC uliofanyika tarehe 15 na 16 Septemba 2017 mkoani Tanga, ulifanya mabadiliko ya katiba yake kuhusu muda wa ukomo wa viongozi wa klabu kuwapo madarakani kutoka miaka mitatu hadi miaka mitano kama inavyoonekana katika katiba ya UTPC kipengele namba 15 (C).

 

Kwa mujibu wa azimio namba 8.3 la Mkutano Mkuu wa dharura uliofanyika Dodoma terehe 23/08/2013, wajumbe waliazimia kwamba klabu zote zifanye uchaguzi wao mapema kabla ya uchaguzi wa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ambapo wajumbe wake huchaguliwa kutoka miongoni mwa viongozi wa juu wa  Klabu za Waandishi wa Habari.

 

Katika kikao cha 33 cha Bodi ya Wakurugenzi kilichofanyika tarehe 20/11/2019 mkoani Dodoma, kilipitisha azimio namba 5.2.4.1 ambalo lilizitaka klabu zote ziwe zimefanya uchaguzi wa viongozi wake mpaka kufikia tarehe 30 Juni 2020 ili kupisha uchaguzi wa Mkuu wa Serikali na uchaguzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC.

 

Hata hivyo kutoka na mlipuko wa ugonjwa wa COVID19, Bodi ilisogeza mbele muda wa chaguzi za klabu mpaka kufikia tarehe 30 Septemba 2020.

 

Baada ya maagizo haya kutolewa na Bodi ya Wakurugenzi, klabu zilianza kufanya chaguzi zake katika vipindi tofauti tofauti, na ifuatayo ni orodha ya klabu ambazo zimeshafanya chaguzi zake;

 

Central Press Club

Kigoma Press Club

Njombe Press Club

Mwanza Press Club

Geita Press Club

Songwe Press Club

Rukwa Press Club

Katavi Press Club

Mara Regional Press Club

Simiyu Press Club

Shinyanga Press Club

Mtwara Press Club

Lindi Press Club

Kagera Press Club

Mbeya Press Club

Arusha Press Club

Manyara Press Club  

 

Klabu zilizobaki bado zinaendelea na mchakato wa kufanya chaguzi zake na pindi wakatakapo maliza taarifa yake itaandaliwa.

Read More